here

Sunday, August 20, 2017

Majibu ya Mbunge Msukuma kwa Tundu Lissu kuhusu Bombardier

Baada ya Serikali kutoa tamko kuhusu ishu ya ndege Bombardier kukamatwa Canada ambayo ilitolewa na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ambaye alisema ndege hiyo imekamatwa na wadeni wanaoidai Serikali.

Leo August 20, 2017 Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Msukuma amemjibu Mbunge Lissu akisema Watanzania wanatakiwa kuendelea kujenga uchumi wa nchi.

”Nimemsikiliza Tundu Lissu lakini tumesikiliza pia majibu ya Serikali yaliyotolewa na Msemaji wa Serikali. Kikubwa ni kuwaomba Watanzania tuendelee kujenga uchumi wetu wa Serikali ya viwanda. Kutoka kwenye uchumi tuliokuwa nao mpaka hapa tulipo na tunakoelekea.

No comments:

Post a Comment