Mbunge viti maalumu mkoa wa Kigoma Josephine Ngezabuke (CCM) amepata ajali mbaya ya gari akitokea Kakonko katika kijiji cha Mvugwe wilayani kasulu mkoani Kigoma Jana majira ya saa kimu na moja jioni.
Hali ya mbunge huyo inaripotiwa sio nzuri, hata hivyo katika ajali hiyo aligongwa mtoto mdogo ambaye ni mwanafunzi na alifariki papohapo, Majeruhi wengine ni Dereva wa CCM Wilaya ya Kasulu (Mzee Saidi) na Diwani mmmoja wa viti maalumu
Mbunge huyo amelazwa katika hospital ya wilaya ya kasulu, inaelezwa kuwa atakuwa ameathirika zaidi Mgongoni na kwamba hawezi hata kukaa.
Hata hivyo kesho Ofisi ya bunge inamtumia ndege maalumu kwaajili kumsafirisha Hospitali kuu ya taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaid
No comments:
Post a Comment